Mzee wa tafakari

Friday, August 10, 2007




Powered By SeeBeforeYouDie.net
Share your Travel Experiance

Wednesday, August 08, 2007

CCM kumfia mikononi Rais Kikwete


WIKI hii Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilifanya maamuzi mazito yakiwemo kuridhia kuwatimua madiwani watano wa chama hicho, kusimamisha viongozi wote wa Jumuiya ya Wazazi, maafisa wengine wa chama kutoka ofisi ndogo Lumumba jijini Dar es Salaam na Makao Makuu Dodoma.

Pia Kamati Kuu katika kikao chake kilichofanyika kuanzia Jumamosi hadi Jumatatu wiki hii, imetangaza kumvua haki ya
kuchaguliwa katika uongozi wa CCM, Thomas Nyimbo, baada ya kuthibitika kuwa tabia na mwenendo wake havifai.

Nyimbo alikuwa ni mmoja wa wagombea wa kiti cha uenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa. Hivi karibuni Nyimbo amekuwa akitoa shutuma nyingi dhidi ya mgombea wenzake.

Wengine waliosimamishwa uongozi na kamati hiyo ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Abiuod Maregesi, Makamu Mwenyekiti wa jumuiya hiyo,Ramadhan Suleiman Nzori, Babilas Mpemba na Katibu Mkuu, Cosmas Hinju, kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu wa fedha za jumuiya hiyo.

Mtu mwingine aliyekutana na makali ya panga la kamati hiyo ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Mujuni Kataraiya ambaye ametagazwa kufukuzwa kazi kutokana tuhuma za ubadhirifu wa mali za chama wakati alipokuwa Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mwanza.

Kwa hakika maamuzi hayo ni mazito kwa chama hicho tawala kuwahi kuyatoa katika siku za hivi karibuni.

Swali tunalojiuliza hivi kweli CCM imeaamua kuzaliwa upya kutokana na kuamua kuanza kuchukua hatua za kuwashughulikia wabadhirifu wa mali zake au ni maamuzi ya kisiasa ambayo yamejifichia katika ubadhirifu?

Nasema hivyo kwa sababu kwa miaka yote CCM ndiyo ambayo ilikuwa chama ambacho kilisifika kutokana na kukumbatia ufisadi, hakuna hatua ambazo zimewahi kuchukuliwa kwa watu ambao wamehusika katika kuua miradi yake mikubwa ya uchumi.

Ilifikia mahali hata watumishi wa serikali waliokuwa wakifilisi mali za umma, badala ya kufukuzwa walipewa ulaji mwingine kwa kupewa mashirika mengine kuyaongoza. Kisa kanda wa CCM!

Leo kufumba na kufumbua tunaona CCM ile ile tuliyoizoea inaibuka na maamuzi mazito kama haya ya kuwatimua kazi wabadhirifu wa mali zake. Kwa hakika umetuachia maswali mengi ya kujiuliza.

Wapo wanaofikiria kuwa uamuzi wa kuwasimamisha viongozi wote wa jumuia ya wazazi ni wa kisiasa zaidi kutokana na juimuia hiyo viongozi wake hawakuwa kambi ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Hisia zilizopo ni kwamba walioadhibiwa katika kikao hicho ni wale tu ambao walionekana kuwa hatari katika ustawi wa mtandao wa Rais Kikwete uliomwigiza madarakani.

Ingawa kamati kuu imetangaza rasmi kuvunja mtandao ndani ya chama hicho lakini ukweli unabaki pale pale kwamba wanaoendelea kumzunguka rais na kumpa ushauri ni wale wale wana mtandao ambao leo ndio wanaomshauri Rais vibaya katika uendeshaji wa uchumi na masuala mengine.

Lakini wana mtandao hao mbali ya kumzunguka rais lakini wana ajenda nyingine ya kutengeneza rais wa Tanzania wa baada ya rais Kikwete kumaliza muda wake.

Dhambi kubwa ambayo imewaponza watu hao walioadhibiwa ni kuwa na mtizamo toafuti ndani ya chama hicho. Ingawa hao wameadhibiwa lakini hiyo imetumika kama njia yakuwatisha wengine ambao wanaonekana kuwa tishjiop la mtandao huo.

Miongoni mwa watu ambao mpaka sasa wanaonekana kukigawa chama kutokana na nguvu walizonazo ambao sio wana mtandao ni pamoja na Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Mark Mwandosya, waziri mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, na waziri wa ardhi na maendeleo ya makazi, John Magufuli.

Kwa hakika nyufa ndani ya CCM bado ni kubwa na kwamba kama hatua za kumaliza makundi ndani ya chama hicho hazitachukuliwa haraka, huenda chama hicho kikamfia mikononi Rais Kikwete kama ataendelea kulea kundi la marafiki zake la wanamtandao.

Wednesday, August 01, 2007

Vitambi vya ukimwi

WIKI hii serikali ilianzisha kampeni maalumu ya
upimaji wa hiyari kujua kama wananchi wameambukizwa
virusi vya ukimwi iliyoongozwa na Rais Jakaya Kikwete
ambaye yeye na mkewe, Salma walipima jijini Dar es
Salaam wakiungwa mkono na mamia ya wakazi
waliojitokeza.

Kampeni hiyo pia ina lengo kuanza kutoa dawa za
kupunguza makali ya ugonjwa huo (ARVs) bure kwa watu
watakaobainika kuwa wameathirika.

Mara baada ya kupima, Rais Kikwete alionyesha majibu
yake dharani ikionyesha kuwa yuko safi na mkewe na
baadhi ya wanasiasa waliopima siku hiyo baadhi yao
walitangaza majibu yao huku wengine wakikaa kimya.
Wengine walikimbia kujitokeza kupima.

Kampeni hiyo ya kupima kwa hiari sasa imeanza kuchukua
sura ya kisiasa zaidi, wengi hasa viongozi wanaotoka
chama tawala wanataka kujitokeza kupima ili
kumwonyesha Rais kwamba wako pamoja naye.

Lakini inawezekana kwamba viongozi wapinzani,
wanajitokeza kupima ili kupata imani ya wananchi kuwa
wako fiti kwa ajili ya kugombea urais katika uchaguzi
ujao.

Wakati kampeni hiyo ikiendelea, baadhi ya wabunge wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati
wakichangia hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara
ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa mwaka wa fedha 2007/8
bungeni Dodoma wameungana na waathirika wa ukimwi
kueleza wasiwasi wao kuhusu udaganyifu uliopo katika
ARVs.

Wabunge wanasema kuwa baadhi ya dawa za ARVs
zimeelezwa kwamba zinasababisha madhara kwa watu
wanaozitumia.

Kwa kifupi ni kwamba fedha kwa ajili ya kununulia dawa
za ARVs zinadaiwa kutumiwa kwa matumizi mengine na
nyingine kuishia kunenepesha matumbo ya wakubwa wa
serikali.

Kutokana na ufisadi mkubwa uliopo katika fedha
zinazotoka kwa wahisani hususan mfuko wa kusaidia
wenye ukimwi (Global Fund), waathirika wanapewa ARVs
ambazo zimekwisha muda wa matumizi yake na nyingine
ambazo haziwapi madhara makubwa.

Baadhi ya dawa hizo zinadaiwa kusababishia athari
mbalimbali watumiaji ikiwamo kukua matiti na makalio,
kuathiri mwenendo wa kula na kuwafanya wawe na matumbo
makubwa kiasi kwamba wanawake huonekana kama
wajawazito na wakati mwingine huwaongezea hamu ya
kushiriki vitendo vya ngono.

Kwa hakika malalamiko haya ni mazito ambayo serikali
inapaswa kuyatolea maelezo ya kina ili wananchi wajue.


Si wabunge wenye hofu kuhusiana na malalamiko hayo,
bali wananchi wote wanataka kujua serikali
imeshushghulikia vipi tatizo hilo na watu wanaokula
fedha za ukimwi.

Ninasema hivyo kwa kutambua jinsi matumizi ya ARV
yalivyo tete na kwa kuzingatia kwamba mtumiaji
anapaswa azitumie kwa maisha yake yote huku
akizingatia masharti na ushauri wa madaktari kuhusu
aina ya vyakula na dawa za kutumia.

Katika mazingira kama hayo mategemeo makubwa ya
mwathirika ni katika matumizi ya ARVs sahihi. Iwapo
ARVs hizo zinaleta madhara, ni wazi kwamba serikali
inawaandalia vifo vya haraka watu hao bila wasiwasi.

Ni vyema sasa kwa Serikali kusikiliza kilio hicho na
kutoa maelekezo sahihi kabla watumiaji hawajaingiwa
woga na kuacha kuzitumia, kama baadhi yao
walivyotishia.

CCM kumfia mikononi Rais Kikwete


WIKI hii Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilifanya maamuzi mazito yakiwemo kuridhia kuwatimua madiwani watano wa chama hicho, kusimamisha viongozi wote wa Jumuiya ya Wazazi, maafisa wengine wa chama kutoka ofisi ndogo Lumumba jijini Dar es Salaam na Makao Makuu Dodoma.

Pia Kamati Kuu katika kikao chake kilichofanyika kuanzia Jumamosi hadi Jumatatu wiki hii, imetangaza kumvua haki ya
kuchaguliwa katika uongozi wa CCM, Thomas Nyimbo, baada ya kuthibitika kuwa tabia na mwenendo wake havifai.

Nyimbo alikuwa ni mmoja wa wagombea wa kiti cha uenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa. Hivi karibuni Nyimbo amekuwa akitoa shutuma nyingi dhidi ya mgombea wenzake.

Wengine waliosimamishwa uongozi na kamati hiyo ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Abiuod Maregesi, Makamu Mwenyekiti wa jumuiya hiyo,Ramadhan Suleiman Nzori, Babilas Mpemba na Katibu Mkuu, Cosmas Hinju, kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu wa fedha za jumuiya hiyo.

Mtu mwingine aliyekutana na makali ya panga la kamati hiyo ni Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Mujuni Kataraiya ambaye ametagazwa kufukuzwa kazi kutokana tuhuma za ubadhirifu wa mali za chama wakati alipokuwa Katibu wa chama hicho Mkoa wa Mwanza.

Kwa hakika maamuzi hayo ni mazito kwa chama hicho tawala kuwahi kuyatoa katika siku za hivi karibuni.

Swali tunalojiuliza hivi kweli CCM imeaamua kuzaliwa upya kutokana na kuamua kuanza kuchukua hatua za kuwashughulikia wabadhirifu wa mali zake au ni maamuzi ya kisiasa ambayo yamejifichia katika ubadhirifu?

Nasema hivyo kwa sababu kwa miaka yote CCM ndiyo ambayo ilikuwa chama ambacho kilisifika kutokana na kukumbatia ufisadi, hakuna hatua ambazo zimewahi kuchukuliwa kwa watu ambao wamehusika katika kuua miradi yake mikubwa ya uchumi.

Ilifikia mahali hata watumishi wa serikali waliokuwa wakifilisi mali za umma, badala ya kufukuzwa walipewa ulaji mwingine kwa kupewa mashirika mengine kuyaongoza. Kisa kanda wa CCM!

Leo kufumba na kufumbua tunaona CCM ile ile tuliyoizoea inaibuka na maamuzi mazito kama haya ya kuwatimua kazi wabadhirifu wa mali zake. Kwa hakika umetuachia maswali mengi ya kujiuliza.

Wapo wanaofikiria kuwa uamuzi wa kuwasimamisha viongozi wote wa jumuia ya wazazi ni wa kisiasa zaidi kutokana na juimuia hiyo viongozi wake hawakuwa kambi ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.

Hisia zilizopo ni kwamba walioadhibiwa katika kikao hicho ni wale tu ambao walionekana kuwa hatari katika ustawi wa mtandao wa Rais Kikwete uliomwigiza madarakani.

Ingawa kamati kuu imetangaza rasmi kuvunja mtandao ndani ya chama hicho lakini ukweli unabaki pale pale kwamba wanaoendelea kumzunguka rais na kumpa ushauri ni wale wale wana mtandao ambao leo ndio wanaomshauri Rais vibaya katika uendeshaji wa uchumi na masuala mengine.

Lakini wana mtandao hao mbali ya kumzunguka rais lakini wana ajenda nyingine ya kutengeneza rais wa Tanzania wa baada ya rais Kikwete kumaliza muda wake.

Dhambi kubwa ambayo imewaponza watu hao walioadhibiwa ni kuwa na mtizamo toafuti ndani ya chama hicho. Ingawa hao wameadhibiwa lakini hiyo imetumika kama njia yakuwatisha wengine ambao wanaonekana kuwa tishjiop la mtandao huo.

Miongoni mwa watu ambao mpaka sasa wanaonekana kukigawa chama kutokana na nguvu walizonazo ambao sio wana mtandao ni pamoja na Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Profesa Mark Mwandosya, waziri mkuu wa zamani, Frederick Sumaye, na waziri wa ardhi na maendeleo ya makazi, John Magufuli.

Kwa hakika nyufa ndani ya CCM bado ni kubwa na kwamba kama hatua za kumaliza makundi ndani ya chama hicho hazitachukuliwa haraka, huenda chama hicho kikamfia mikononi Rais Kikwete kama ataendelea kulea kundi la marafiki zake la wanamtandao.