Mzee wa tafakari

Tuesday, February 06, 2007

Msabaha maafisa Tanesco kufanyakazi saa 24 kusimamia

WIKI hii Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha aliwasha moto ndani ya Shirika la Umeme (Tanesco) kuwataka mabosi wa shirika hilo kuongeza muda wa kazi kwa ajili ya kusimamia ratiba ya mgawo wa umeme.

Kutokana na amri hiyo mameneja wa mikoa wa Tanesco wameamriwa kukaa ofisini hadi saa 2.00 usiku kufuatilia ratiba ya mgawo ili pale linapotokea tatizo wakati wa kurudisha umeme kwa watumiaji wadogo waweze kulishughulikia haraka.

Dk Msabaha ameuagiza uongozi wa Tanesco kuhakikisha makao makuu ya shirika kunakuwepo na maafisa saa 24 kupokea taarifa za watumiaji wa umeme.

Waziri anasema amelazimika kutoa maagizo hayo kuhakikisha umeme mdogo unaopatikana unagawiwa kwa haki na unatumiwa vizuri ili kukidhi mahitaji ya watumiaji wakubwa na wale wadogo.

Waziri Msabaha pia ameagiza makao makuu ya shirika hilo kuunda timu itakayosimamia na kufanya ukaguzi wa dharura kuona kama mgawo huo unatekelezwa na maafisa wa shirika hilo.

Nakubaliana na waziri Msabaha kabisa kuwa hivi sasa wakati wa mgawo wa umeme watu wote bila kubagua wanapaswa kupata mgawo sawa bila ya kuwepo upendeleo.

NI kweli pia kuwa nchi ipo katika matatizo makubwa ya ukame wa muda mrefu ambao umesababisha uzalishaji katika vyanzo vya umeme kupungua sana na hivyo kuzalisha umeme chini ya viwango kinachotakiwa.

Hata hivyo, uamuzi wa kulazmisha maafisa wa makao makuu ya TANESCO kukaa muda saa 24 ofisini kwa ajili ya kuangalia mgawo wa ume

Serikali kupitia Shirika lake la Umeme (Tanesco) limeanza kuachana na utegemezi nguvu za maji kama
chango umeme kwa kubuni vyanzo mbadala vitakavyozalisha umeme wa kutosha na kusaza.

Chini ya mpango huo muda mfupi na muda mrefu ambao utekelezaji wake umeanza mwezi huu, ifikapo Desemba
mwaka huu, shirika hilo litakuwa linapata megawati 528 za umeme bila kutegemea nguvu za maji, ikiwa ni
pungufu kidogo ya jumla ya umeme unaohitajika nchini wa megawati 560.

Mkurugenzi wa Uzalishaji Umeme wa Maji wa Tanesco, Declan Mhaiki, alithibitisha jana kuwepo kwa mpango
huo na kwamba tayari baadhi ya zabuni zimeshafunguliwa ili kuruhusu kuanza utekelezaji wake.

Hata hivyo, alisema sambamba na mpango huo, shirika halitaachana kabisa na umeme wa maji, lakini uwekezaji
katika umeme, hivi sasa utalalia katika vyanzo vingine, hasa gesi asilia ili kupata umeme wa uhakika,
badala ya huu wa kutegemea mvua za mashaka.

Mhaiki, alisema kwa sasa shirika lake linanunua umeme wote unaozalishwa na IPTL na Songas wa megawati 283 na
ifikapo Agosti mwaka huu, litakodisha mitambo ya dharura ya kuzalisha umeme wa kutumia gesi wa megawati
100. Zabuni zake zilifunguliwa Jumatatu iliyopita.

Alisema pia kuwa Tanesco Machi 13, mwaka huu ilifungua zabuni za kufunga mitambo ya kuzalisha megawati 60
nyingine za umeme wa kutumia gesi asilia katika kituo cha Ubungo na mingine ya megawati 40 katika kituo cha
Ilala, ambayo itakuwa tayari Desemba mwaka huu.

Chini ya mpango huo, Tanesco imedhamiria kuwa ifikapo Desemba mwaka huu, mitambo ya kuzalisha megawati 45
kwa kutumia gesi asilia iwe imefungwa Tegeta na kufanya umeme utakaozalishwa ndani ya mkakati huo
kufikia megawati 528, bila kuingiza umeme unaozalishwa na kwa nguvu za maji.

Katika mpango wake wa muda mrefu, Tanesco inakusudia kufunga mitambo mingine ya gesi asilia itakayofungwa
Kinyerezi Jijini Dar es Salaam ili kuzalisha megawati 200 ifikapo mwaka 2009 na baadaye kuunganisha gridi ya
Taifa na Zambia ili kununua megawati 200 zaidi za umeme ifikapo mwaka 2010.

Endapo mikakati hiyo itafanikiwa, ndani ya miaka mitano ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete, Tanzania
itaweza kupata megawati 928 za umeme karibu mara mbili ya umeme unaohitajika nchini.

Akithibitisha kuwa umeme wa maji hajautupwa kabisa, Mhaiki, alimweleza Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed
Shein, aliyetembelea bwawa la Mtera jana, kuwa ifikapo mwaka 2012 serikali itakuwa imejenga kituo kipya cha
kuzalisha umeme wa nguvu za maji katika mto Ruhdji kitakachozalisha megawati 358.

Mpango huo wa serikali umekuja baada ya kukosekana kwamatumaini katika umeme unaotegemea nguvu za maji hasa baada ya kukosekana kwa mvua kwa kipindi kirefu.

Mfano, bwawa la Mtera ambalo kwa hali yake ya kawaida huzalisha megawati 80, limekauka na kufikia katika
kiwango kisichoruhusiwa kutumika, lakini kwa kuwa majiyake baadaye hutumika kuzalisha umeme Kidatu mkoani
Morogoro, inabidi kuzalisha umeme usiozidi megawati 20 kwa siku ili kuruhusu maji kwenda Kidatu.

Hata mvua zinazoendelea kunyesha katika mikoa ya Dodoma, Mbeya na Iringa hazijaleta matumaini yoyote
kwani hadi jana maji yameongezeka kwa sentimita takriban 30, kufikia mita 687.68 tangu mwishoni mwa
Februari.

Mwenendo wa kupungua kwa kina cha maji hayo unatia shaka zaidi kwani kwa miaka mitano iliyopita, maji
yanayoingia bwawani humo yamepungua kutoka mita za ujazo 139 kwa sekunde mwaka 2001 hadi mita za ujazo 41
kwa sekunde mwaka jana.

Kwa mujibu wa meneja wa Kituo cha kuzalisha umeme cha Mtera, Nazir kachwamba, maji hayo mwaka huu yamefikia
kiwango cha chini kabisa ambacho hakikuwahi kufikiwa kwa miaka 20.

0 Comments:

Post a Comment

<< Home